Wednesday, May 16, 2018

KIBA AKING'ANG'ANIA KISWAHILI

Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini Ali Saleh Kiba ( Alikiba) ameonyesha kujali na kuthamini lugha ya kiswahili kupitia kazi zake za sana ya muziki.


Kiba amebainisha haya hivi punde alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari “Lugha yetu ni nzuri lazima tujivunie, najivunia sana kuwa mswahili na kuongea Kiswahili na kutumia kiswahil katika kazi yangu ya kunipatia maisha, kwahiyo kila mtanzania ni lazima ajivunie kuwa mswahili, asikwambie mtu acha uswahili, ni lazima ujivunie sio sifa mbaya” amesema kiba

Pia  amesema kwamba hata akiwa anafanya matamasha nje ya nchi idadi kubwa ya watu  wamekuwa wakitamani kufundishwa lugha ya kiswahili.

No comments: