Sunday, February 11, 2018

11 February 2018,Elizayo Unique -Nahitaji management iliyojitosheleza

Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka  Jijini Mwanza hapa nchini Elizayo Unique aonyesha kuhitaji usimamizi mzuri wa kazi za muziki wake

Elizayo ameyasema haya  leo wakati akifanya mahojiano na Tovuti hii "
Management ilio jitosheleza naamini inaweza kunifikisha katika safar yangu ya mziki",.

"Ugumu ninaoupata nakosa Bageti iliyojitosheleza kwa 100% ili kuipromote Nazi yangu kuna Media nchini  nakosa nguvu kwasababu mziki biashara ili wimbo upigwe kwa kasi inabidi uwe na bajeti iliyokamilika",.amesema

Aidha  ameeleza muda aliotumia kua ndaa wimbo wake mpya wa Bye Bye kuwa alitumia   muda wa mwaka mmoja mpaka kuuachia 

Pia amefafanua juu ya maudhui ya wimbo wa Bye Bye  kuwa ni ushauri kwa wakinadada waongo na wenye michepuko nje ya Mapenzi yao pamoja na umbea 

Amemalizia kwa kuwashauri wanawake wauache  mchepuo wa mapenzi na waseme bye bye watulie katika mahusiano yao.

Wimbo wa Elizayo  Bye Bye unapatikana katika Tovuti za muziki hapa nchini 

No comments: