Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) George Masaju amesema ofisi yake imeokoa Sh156 bilioni ambazo zingetumika kwa ajili ya uchaguzi wa marudio kama serikali ingeshindwa na kurudia kufanya uchaguzi katika majimbo 52.
Masaju amesema hayo wakati wa mkutano wa baraza la wafanyakazi wa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali.
Masaju amesema kiasi hicho kiliokolewa baada ya serikali kushinda kesi 52 kati ya 53 zilizofunguliwa kupinga ushindi wa wabunge na kutaka uchaguzi urudiwe.
Kwa tafsiri hiyo gharama za uchaguzi kwa mujibu wa AG kwa jimbo moja itakuwa ni Sh3 bilioni kiasi kinachoelezwa kuwa ni kikubwa kwa uchumi wa nchi.
Masaju ambaye ni mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi wa ofisi ya mwanasheria, amesema kiasi hicho kiliokolewa baada ya ofisi yake kusimamia weledi na taaluma na haki ikapatikana kwa serikali.
No comments:
Post a Comment