Monday, December 18, 2017

18 December 2017,Baraza la usalama la umoja wa mataifa kujadili juu ya Jerusalem

Baraza la Umoja wa Mataifa kukutana leo hii kujaidili suala la Jerusalem na hatma yake baada ya rais wa Marekani kutangaza kuwa mji huo ni mji mkuu wa Israel.

Suala litakalo jadiliwa katika mkutano huo wa Baraza la Usalama ni hatma ya jiji la Jerusalem na kutolea wito mataifa kutohamisha balozi zao mjini Jerusalem.

Makubaliano kuhusu maazimio yaliochukuliwa kuhusu jiji la Jerusalem yanatakiwa kuheshimishwa.

Wizara ya mambo ya nje ya Uturuki ilifahamisha Jumapili kuwa Jumatatu kutafanyika mkutano wa kuhusu Jerusalem na ukiukwaji wa makubaliano ya Umoja wa Mataifa.

Uamuzi wa Marekani kutangaza kuutangaza mji wa Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel hauna maana yeyote.

Mkutano huo wa Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa umetolewa wito na Misri baada ya Palestina kutama waraka wake.

Ikumbukwe kuwa Marekani ina kura ya turufu katika Baraza la Usalama jambo ambalo linaonekana kuwa suala la Jerusalem litafikishwa katika Umoja wa Mataifa na kutatuliwa na wanachama wote.

No comments: