Wednesday, November 29, 2017

29 November 2017,Waziri mkuu abaini jumla ya malori 44 yaliyokuwa yanatolewa kimagendo bandarini

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Novemba 29, 2017  amefanya ziara ya kushtukiza katika bandari ya Dar es salaam na kubaini malori 44  yaliyokuwa yakitaka kutolewa bandarini hapo bila ya kufuata utaratibu.
Akiwa bandarini Waziri Mkuu Majaliwa amewataka mawakala kuwa makini na watu wanaowarubuni wawasaidie kupitisha mizigo kwa kutaja majina ya viongozi wakuu wa serikali.

No comments: