Wednesday, November 29, 2017

29,November 2017, watu 40 wameuawa ,19 kujeruhiwa na wezi wa zaidi ya mifugo 1,000 Sudan kusini


 watu 40 wameuawa  na   19 kujeruhiwa na wezi walioiba zaidi ya mifugo  1000    siku moja kabla  ya leo  Sudan kusini   
Kwa mujibu wa taarifda zilizotolewa na serikali watu 40 wameuawa na wengine 19 wamejeruhiwa na wezi wa mifugo baada ya kuvamiwa Jumanne katika mkoa wa Jongleri.
Taarifa zinafahamisha kuwa ghasia zinazidi kuongezeka katika eneo hilo.
Waziri wa habari wa Sudani Kusini Jacob Akech Dengdit ameafahamisha kuwa wezi hao wamesababisha vifo vya watu 40 na kuwateka wengine kadhaa.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa ni kwamba watu hao waliokuwa na silaha walitokea katika eneo la Boma.
Wahalifu hao wanaonekana kuwa na lengo la kufifiza zoezi la serikali ya Sudani Kusini ya kurejesha amani ya kudumu.
Mara kwa mara wahalifu kutoka Murle Boma wamekuwa wakivamia raia na kuwapora mali na mifugo yao.
Zaidi ya mifugo  1 000 imeibiwa huku watoto na wanawake wakitekwa na wahailifu hao.

No comments: