Wanajeshi wa Marekali na Niger wafariki katika shambulizi la kushtukiza lililotekelezwa katika eneo la mpakani na Mali.
Taarifa zinafahamisha kuwa makabiliano kati ya wanajeshi na kundi la waasi bado yanaendelea.
kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyanzo vya habari ni kwamba shambulizi hilo lilitekelezwa Jumatano wakati wanajeshi hao walikuwa wakijaribu kuendesha operesheni dhidi ya waasi hao.
Operesheni hiyo ilitekelezwa katika eneo la Niger mpakani mwa Mali.
Hakuna taarifa zaidi iliotolewa kuhusu idadi ya wanajeshi waliofariki.
Jeshi la AFRICOM na lile la Niger limethibitisha tukio hilo.
No comments:
Post a Comment