Monday, October 30, 2017

30 October 2017,Rais Magufuli awapongeza waliovunja nyumba ya CCM Jijini Mwanza

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amewapongeza viongozi waliohusika kuvunja nyumba ya CCM iliyokuwa imejengwa katika hifadhi ya barabara jijini Mwanza.

Rais Magufuli ametoa pongezi hizo leo alipokuwa akizindua daraja la kisasa la waenda kwa miguu la Furahisha jijini humo.

“Ile nyumba moja ya CCM nayo ilikuwa kwenye road reserve (hifadhi ya barabara).

Nawashukuru viongzi wa mkoa kwa kulibomoa. Maendeleo yana madhara yake. Kwahiyo, nawashukuru Mkuu wa Mkoa, mmefanya vizuri sana,” alisema Rais Magufuli.

No comments: