Monday, October 30, 2017

30 October 2017,Waziri Mkuu kushughulikia migogoro ya wafugaji Mkoani Arusha

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amewataka wafugaji wa Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha kuwa watulivu wakati suala la mgogoro kati yao na hifadhi likiwa linashughulikiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Naibu Waziri Ulega ameeleza hayo jana katika mkutano na wafugaji hao uliofanyika kwenye Kata ya Ololosokwan wilayani humo.

Amesema Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli ni inawajali watu wanyonge hivyo wafugaji hao wavulimie na kwamba timu iliyoundwa na waziri mkuu siku za nyuma iliwashirikisha baadhi ya viongozi wao wakiwamo madiwani.

No comments: