Kocha wa Monaco, Leonardo Jardim, kocha wa Ujerumani, Joachim Low, kocha Mkuu wa Celtic, Brendan Rodgers na kocha wa Manchester City, Mikel Arteta ni miongoni mwa watu awali walioorodheshwa kuwania mikoba ya Arsene Wenger
Hata hivyo kama tathmini itakayofanywa mwishoni mwa msimu huu itaridhisha, Wenger ambaye nafasi yake iko hatarini baada ya kipigo cha Jumapili katika fainali ya Carabao Cup kutoka kwa Manchester City, atalazimika kupambana ili kumalizia miezi yake 12 ya mkataba wake.
Lakini inavyoonekana sasa ndani ya Arsenal nguvu ya kumng’oa Wenger klabu hiyo ya Kaskazini mwa London mwishoni mwa msimu ni kubwa.
Tathmini ya mwishoni mwa msimu ndio itabeba mustakabali wa Wenger kama apewe nafasi nyingine ya kubaki kwa msimu mwingine au aondolewe.
No comments:
Post a Comment