Monday, February 19, 2018

19 February 2018,Eden Hazard afurahia kuwa Stamford Bridge

Mchezaji wa Chelsea mbelgiji Eden Hazard, 27, anasema yuko na furaha huko Stamford Bridge lakini hajasema kuwa hatakihama klabua hiyo siku za usoni. (Telefoot - in French)

Meneja wa zamani wa Chelsea Carlo Ancelotti hana fikra za kurudi Paris St-Germain kwa sababu anataka kurudi kwa Premier League. (Mirror)

Leicester wametuma maajenti kumtazama beki wa Benfica Andre Almeida, 27, na wing'a Rafa Silva, 24. Wachezaji wote hao walihusishwa na Leicester mwezi Januari. (O Jogo via Leicester Mercury)

AC Milan na Inter Milan wana nia ya kumsaini mshambuliaji Mario Balotelli, 27, kutoka Nice. Raia huyo wa Italia amekasirishwa kwa kupewa kadi ya njano wakati akimlalamikia refa kuhusu kisa ya ubaguzi wa rangi. (Sun)

Kiunga wa kati ya Manchester United Paul Pogba, 23, amerejea kwenye mazoezi baada ya kuwa mgonjwa kabla ya mechi ya Jumamosi ya kombe la FA ambapo Man United walipata ushindi dhidi ya Huddersfield. (Mail)

Real Madrid wanataka kumuuza kwa zaidi ya pauni milioni 100 kwa wing'a Gareth Bale ili kumununua mashambulizi wa Chelesea Eden Hazard, 27. (Sunday)

Chelsea watamuuliza mshambulizi raia wa Argentina Sergio Aguero, 29, ikiwa Manchester City iliongea na Hazard. (Star

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho alijibizana na kiungo wa kati mfaransa Paul Pogba na mlinzi raia wa England Phil Jones baada ya kikosi chake kulimwa na Newcastle wiki iliyopita. (Sun on Sunday)

Mourinho alifanya mkutano wa saa moja kukana tofauti zake na Pogba.

No comments: