Sunday, February 18, 2018

18 February 2018,Wapalestina kadha wauawa baada ya Israel kushambulia Gaza

Wapalestina wawili wameripotiwa kupoteza maisha baada ya Israel kufanya mashambulizi Gaza.

Kwa mujibu wa habari,jeshi la Israel limeshambulia ngome za Hamas katika ukanda wa Gaza na kusababisha vifo vya wapalestina wawili huku wengine wakiwa wamejeruhiwa.

Msemaji wa wizara ya afya nchini Palestina amesema kuwa majeruhi hawapo katika hali mbaya.

Jeshi la Israel nalo limeripoti kuwa askari wake wanne walijeruhiwa baada ya mlipuko kutokea karibu na kusini mwa mpaka wa Gaza na Israel.

Israel inaamini kuwa Hamas ndio wanahusika na kutokea kwa mlipuko huo.

No comments: