Klabu ya soka ya Yanga imefanikiwa kuingia hatua ya 16 bora ya michuano ya kombe la shirikisho nchini baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 6-5 kupitia mikwaju ya Penalti dhidi ya Ihefu FC.
Yanga iliwabidi kusubiri hadi dakika za majeruhi kusawazisha bao la mapema la Ihefu FC inayoshiriki ligi daraja la pili, kupitia mkwaju wa penalti uliopatikana baada ya Chirwa kuangushwa kwenye eneo la hatari ambapo alipiga mwenyewe na kufunga.
Baada ya timu hizo kutoka sare ya 1-1 ndani ya dakika 90 mwamuzi akaamuru mikwaju ya penalti ambapo Yanga wameibuka na ushindi wa jumla ya 6-5.
Nyota wa Yanga raia wa Zambia Obrey Chirwa alikosa mkwaju wake kabla ya golikipa Youthe Rostand kusawzisha makosa yake.
Yanga sasa inaungana na timu zingine zilizoshinda katika hatua ya 16 bora ikiwemo Azam FC ambayo mapema imesonga mbele baada ya kushinda 5-0 dhidi ya Shupavu FC ya Morogoro.
Matokeo katika mechi zingine.
Mwadui FC 1-2 Dodoma FC
Kagera Sugar 0-2 Buseresere
Kariakoo Lindi 0-1 Mbao FC
No comments:
Post a Comment