Kufanikiwa kwa Arsenal kumnunua mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang kwa £60m kutategemea makubaliano kuhusu wachezaji wengine wawili.
Na mshambuliaji wa Gunners Olivier Giroud ndiye huenda akawa na usemi zaidi kuhusu iwapo mkataba wa kuhama kwa Aubameyang utakamilishwa kabla ya muda wa mwisho wa kuhama wachezaji kipindi hiki, Jumatano saa 23:00 GMT.
Arsenal wamekubali kulipia gharama na mikataba ya kibinafsi ya mchezaji huyo kutoka Gabon mwenye umri wa miaka 28.
Lakini Dortmund itaidhinisha hatua hiyo kama watapata mchezaji wa kuchukua nafasi yake.
No comments:
Post a Comment