Sunday, January 28, 2018

28 January 2018,Serikali yazitaka Kaya 83 zilizovamia Hifadhi ya Ngorongoro kuondoka

Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangallah amezitaka kaya 83 zinazodaiwa kuvamia eneo la serikali la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kujiandaa kuondoka.

Akizungumza na waandishi leo Januari 28 baada ya kutembelea eneo hilo la Njiro, Kigwangallah amesema ana taarifa viwanja hivyo waliuziana maafisa wa Serikali bodi la Utalii na Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kinyume cha sheria.

"Katika eneo tumepewa taarifa waliopewa viwanja wapo mawaziri wakuu wastaafu wawili ,viongozi wa serikali wastaafu na tayari tumewasiliana na Waziri wa ardhi kupata nyaraka zao" amesema

Katika eneo hilo, kuna nyumba za wakuu kadhaa wa mikoa wastaafu, viongozi wa taasisi za serikali wastaafu na wafanyabiashara kadhaa.

Awali Meneja wa huduma za sheria wa Ngorongoro, Egudius Mweyunge amesema NCAA ilinunua eneo hilo mwaka 2006 kutoka tume ya ubinafsishaji mashirika ya umma(PSRC) mwaka 2006 ekari 40 kwa Sh1.8bilioni.

Hata hivyo amesema baada ya kutaka kuendeleza eneo walikuta tayari halmashauri ya jiji la Arusha wamegawa viwanja 83 tangu mwaka 1996.

"Tulipowafuata jiji wakakiri wamefanya makosa na watatufidia eneo jingine lakini tumeshindwa kufikia muafaka" amesema Meneja huyo

Awali Mhifadhi mkuu wa Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro Dk Fredy Manongi amesema eneo walilovamiwa ni mali ya NCAA na wana mikakati ya kuwekeza.

Admit Mwananchi

No comments: