Mkufunzi wa Chelsea Antonio Conte anataka kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez mwezi Januari , akisema mchezaji huyo, 29 anaweza kuwa ''uwekezaji mzuri''. (Telegraph)
Tottenham iko tayari kufutilia mbali hamu ya kutaka kumsajili winga wa Bordeaux Malcom kwa sababu klabu hiyo ya Ufaransa inaitisha dau la £45m ili kumunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20- ijapokuwa Arsenal bado ina hamu ya kumsajili mchezaji huyo wa Brazil (Mail)
Tottenham iko tayari kuanza mazungumzo ya malipo ya mshambuliaji Harry Kane, 24, huku ikijiandaa kumuongezea kandarasi kiungo wa kati Christian Eriksen, 25, na mshambuliaji Son Heung-min, 25. (Times - subscription required)
No comments:
Post a Comment