Saturday, December 23, 2017

23 December 2017,Waziri wa ulinzi atia maguu Kongo kuwaona wanajeshi wa JWTZ

Ikiwa zimepita siku 16 tangu kuuawa kwa askari 14 wa Jeshi laWananchi Tanzania (JWTZ) waliokuwa kwenye  oparesheni ya ulinzi wa amani katika Jamhuriya Kidemokrasia ya Congo, Waziriwa Ulinzi wa Tanzania Husssein Mwinyi  amewatembelea wanajeshi wa Tanzaenia waliopo nchini humo.

Mwinyi alifika nchini humo December 22, 2017 ambapo  alipowatembelea Wanajeshi wa Tanzania wanaoshiriki katika kikosi cha kimataifa cha kulinda amani mashariki ya Congo, na kuwatembelea wanajeshi waliojeruhiwa wakati wa shambulizi la December  7, 2017.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Beni, Mwinyiametoa wito wa kudumisha ushirikiano kati ya pande zote zinazoshiriki katika kuleta amani Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Wanajeshi 14 wa Tanzania wa kikosi maalum cha nchi za Kusinimwa Afrika SADC waliuawa na wengine 44 kujeruhiwa wakati wamajibizano ya risasi na waasi wasiojulikana katika kambi yao huko Semulik, karibu na mji wa Beni.

No comments: