Tuesday, November 21, 2017

21 November 2017,NEC yakaa mkao wa kula leo Jijini Dar es salaam

Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) imekutana jijini Dar Es Salaam chini ya Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Rais Dkt. John Magufuli.

Katika mkutano huo baadhi ya wanachama waliokuwa katika vyama mbalimbali vya siasa wamezungumza na kuomba ridhaa ya mkutano huo kujiunga na CCM.

Waliotangaza kujiunga na chama hicho kwenye mkutano huo kutoka ACT WAZALENDO ni pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo, Albert Msando, Samson Mwigamba na Edna Sunga.

Lawrence Masha aliyejiondoa hivi karibuni kutoka CHADEMA na Patrobus Katambi aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA - BAVICHA.

Halikadhalika aliyekuwa mwanachama wa CCM, Sophia Simba ameandika barua ya kuomba radhi na kukubaliwa kurejeshwa ndani ya chama hicho.

NEC imewakubali wote walioomba kujiunga na chama hicho.

No comments: