Saturday, November 18, 2017

18 November 2017,Matokeo ya EPL michezoni leo jumamosi

Arsenal ilifunga mabao mawili ya kipindi cha kwanza na kuwalaza wapinzani wao wa jadi mjini London Tottenham kwa mara ya kwanza katika mechi saba za ligi ya Uingereza.

Beki Shkrodan Mustafi alifunga kichwa kizuri kutoka kwa krosi iliopigwa na Mesut Ozil , lakini Spurs wanadai kwamba mpira wa adhabu uliopigwa baada ya Davinson kumchezea visivyo Alexis Sanchez ulikuwa uamuzi mkali.
The Gunners waliongeza bao la pili dakika tano baadaye , baada ya mshambuliaji wa Chile Sanchez kufunga krosi iliopigwa na Alexandre Lacazzette akiwa amekaribia goli.

Sanchez alikuwa na fursa ya kuongeza bao la tatu lakini shambulio lake likapanguliwa na Hugo Lloris.

Fursa nzuri ya wageni hao ilimwangukia kiungo wa kati Christian Eriksen katika kipindi cha kwanza lakini shambulio la kimo cha paka la raia huyo wa Denmark liligonga chuma cha goli huku kipa Petr Cech akiruka na kuokoa kichwa kilichopigwa na Eric Dier.

Ushindi huo sasa umeifanya Arsenal kupanda hadi katika nafasi ya tano katika jedwali la ligi wakiwa na pointi moja juu ya kikosi cha Mauricio Pochettino.

Katika mchezo mwingine Manchester City ilionyesha  uwezo mzuri katika ushindi dhidi ya Leicester ambao umeimarisha uongozi wake katika kilele cha jedwali la ligi ya Uingereza.

Kikosi cha Pep Guradiola kiliendeleza msururu wake wa matokeo mazuri baada ya likizo ya mechi za kimataifa kwa kujipatia ushindi wa 16 mfululizo katika mashindano yote kupitia uongozi wa mshambuliaji wao Gabriel Jesus kabla ya kiungo wa kati De Bryuine kufunga mkwaju mkali ambao kipa wa Leicester alishindwa kuuona.

Wakati huohuo mabingwa watetezi Chelsea walipata ushindi rahisi dhidi ya West Brom na kumuongezea presha kocha wa West Brom Tony Pulis.

Alvaro Morata alifunga bao lake la nane katika ligi baada ya kufunga mpira uliopanguliwa na kipa Ben Foster kufuatia shambulio la Eden Harzard.

Hazard alifunga bao la pili muda mfupi baadaye wakati alipochukua pasi ya kisigino ya Morata, akamchenga Foster na kucheka na wavu kabla ya Marcos Alonzo kufunga bao la tatu kutoka mkwaju wa adhabu wa Cesc Fabregas.

Katika kipindi cha pili Harzard alifunga bao lake la pili kutoka maguu 18 baada ya kupata pasi nzuri kutoka kwa fabregas.

Kwengineko Mohamed Salah aliendeleza umahiri wake kwa kuipatia Liverpool mabao mawili huku timu hiyo ikiilaza Southampton kwa urahisi na kujipatia ushindi wa tatu mfululizo kwa mara ya kwanza 2017.

Baada kuonyesha mchezo mzuri kutoka dakika za kwanza ,mshambuliaji wa Misri Salah alifunga bao zuri kutoka miguu 18 ,baada ya Dusan Tadic kufanya masihara na kupoteza mpira karibu na eneo hatari.

Mshambuliaji huyo aliipatia timu hiyo ya nyumbani bao la pili kufuatia pasi ya Phillipe Coutinho.

Hakuna mchezaji wa ligi ya Uingereza mwenye mabao mengi katika mashindano yote kama Salah msimu huu na ijapokuwa alitulia baada ya kipindi cha kwanza Coutinho alichukua uongozi na kufunga kufuatia mpira uliopanguliwa na kipa baada ya shambulizi la Roberto Firmino.

No comments: