Sunday, October 22, 2017

22 October 2017,Makonda akabidhiwa magari 15 ya Polisi

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  PAUL MAKONDA amekabidhiwa magari 15 ya polisi yaliyokuwa yakitengenezwa Mkoani Kilimanjaro.

MAKONDA amesema amefikia hatua hiyo baada ya kuona changamoto zilizokuwa zikiwakabili polisi katika mkoa wake kutokana na aina ya magari waliyokuwa wanatumia.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya DSM, LAZARO MAMBO SASA amesema kuwa uvumbuzi wa tatizo hilo la magari utasaidia katika doria na ukaguzi wa polisi kwani yametengenezwa maalumu kwa kazi hiyo.

Naye Mkurugenzi wa RSA, MANMOHAM BHAMRAH amesema anamshukuru Mkuu wa Mkoa wa DSM PAUL MAKONDA kwa kumpa nafasi hiyo ya kutengeneza magari kupitia kampuni yake.

Magari ishirini na sita yalipelekwa mkoani Kilimanjaoro kwa jaili ya matengenezo ambapo magari 15 yamepona kabisa na tayari yamekabidhiwa kwa Mkuu wa Mkoa huku magari 11 yakishindikana.

No comments: