Saturday, October 21, 2017

21 October 2017, Watu watano wafariki kwa ajari Kagera

Watu watano wamekufa baada ya gari dogo la abiria aina ya Toyota Hiace kugongana na lori la mizigo katika eneo la Kasharunga barabara kuu ya Muleba –Biharamulo mkoani Kagera na kusababisha kulipuka kwa moto ulioteketeza magari hayo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustino Ollomi amewataka madereva wanaoendesha vyombo vya moto kuongeza umakini wanapokuwa barabarani.

Chanzo cha ajali hii iliyokatisha uhai wa watu watano kinaelezwa kuwa ni mwendo kasi wa gari dogo la abiria aina ya Toyota Hiace lenye namba za usajili T 470 Dey lililokuwa likitoka Muleba mkoani Kagera kugongana na Lori lililokuwa limebeba shehena ya mahindi kuelekea nchini Uganda .

Inasemekana dereva wa gari dogo Magesa Masolele ambaye kwa sasa ni marehemu, alitaka kulipita trekta lililokuwa mbele yake akiwa katika mwendo mkali na kisha kukutana uso kwa uso na lori lenye nambari za usajili T 214 AJD na kusababisha kulipuka kwa moto ambao umekatisha maisha ya abiria watatu ,kondakta na dereva wa Hiace hiyo huku dereva wa lori pamoja na

No comments: