Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesimamisha matangazo ya radio moja inayomilikiwa na Chama cha Wafanyabiashara wa Burundi, kwa kukosoa mauaji ya wakimbizi Warundi waliouawa hivi karibuni na wanajeshi wa DRC.
Eddy Claude Nininahazwe, Mkurugenzi wa CCIB FM+ amesema idhaa hiyo imefungiwa matangazo kwa kupeperusha tahariri iliyokosoa vikali mauaji hayo sambamba na kimya cha vyombo vya dola kuhusu ukatili huo.
Baraza Taifa la Mawasiliano la Kongo DR limehalalisha hatua ya kufunga idhaa hiyo kwa miezi mitatu kuanzia Jumatatu ijayo, likisema kuwa ilikiuka maadili na kanuni za uandishi wa habari.
Septemba 15, waandamanaji 36 ambao walikuwa ni wakimbizi kutoka Burundi walipigwa risasi na kuuawa na wanajeshi katika mji wa Kamanyola mkoani Kivu ya Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Serikali ya Burundi imetaka kufanyika uchunguzi wa kina huku ikiwaomba viongozi wa Kinshasa wawasilishe maelezo kuhusu mauaji hayo.
Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa, wakimbizi wa Burundi elfu 44 wamepewa hifadhi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
No comments:
Post a Comment