Friday, September 29, 2017

29 September 2017,Shule 11 kati ya Shule 300 zilizokuwa zimefungiwa zaanza usajiri

WAMILIKI wa Shule binafsi 11 kati ya shule zaidi ya 300 zilizofungiwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala wamejitokeza kukamilisha usajili pamoja na taratibu nyingine ili waweze kuendelea kutoa elimu.

Shule hizo za awali na msingi ni zile zilizofungiwa tangu Agosti 16 mwaka huu baada ya kubainika kujiendesha kinyume cha sheria ikiwemo kukosa usajili na kutokuwa na eneo la kutosha kuendeshea shule hizo.

Mbali na hayo shule hizo pia zilibainika kubadilisha matumizi ya usajili kwani kuna ambazo zilisajiliwa kama ‘Day care’ lakini wamiliki wakabadilisha na kuzifanya kuwa ‘Nursery’ jambo ambalo ni kinyume cha usajili hivyo kupelekea kufungiwa mpaka hapo wamiliki watakapofuata utaratibu.

Akizungumza na gazeti hili jana Ofisa Habari wa Manispaa hiyo, Tabu Shaib alisema shule 11 tayari zimeanza kusajili ili kuendelea na ufundishaji. Alisema shughuli hiyo ni endelevu na sasa inafanywa na wenyeviti wa kata katika maeneo yote. Aliwataka wamiliki ambao wanajua kuwa shule zao haziendeshwi kwa kufuata sheria.

No comments: