Maafisa usalama nchini Somalia wanasema mlipuko wa bomu la kwenye gari katika mji mkuu Mogadishu umewaua takriban watu saba na kuwajeruhi wengine sita.
Msemaji wa utawala wa Mogadishu Abdifatah Omar Halane ameiambia Sauti ya Amerika-VOA kwamba gari lililipuka Alhamisi karibu na kituo cha basi chenye harakati katika wilaya ya Hamarweyne.
“Kilichotokea ni bomu la kwenye gari lilipiga basi dogo watu saba wameuwawa na wengine sita kujeruhiwa Halane ameiambia VOA”.
Mashahidi kadhaa wameiambia VOA kwamba waathirika walikuwa ni raia wa nchini humo kutoka katika kituo cha basi na eneo la karibu.
Lengo maalum la mlipuko huo bado haliko bayana lakini walioshuhudia wanasema magari ya majeshi ya usalama ya serikali yalikuwa yanapita wakati mlipuko ulipotokea.
Hakuna aliyedai kuhusika na shambulizi.
No comments:
Post a Comment