Mahakama ya Kimataifa ya Kudumu ya Watu wa Malaysia imetoa hukumu dhidi ya serikali ya Myanmar kutokana na kutenda jinai za mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya.
Mahakama hiyo ambayo kuanzia siku ya Jumatatu hadi Ijumaa ya jana ilikuwa ikichunguza vitendo vya ukandamizaji wa serikali ya Myanmar na mauaji dhidi ya Waislamu hao, imeipata na hatia serikali ya Naypyidaw kwa kuhusiaka na jinai hizo.
Uamuzi wa mahakama hiyo uliotolewa na majaji saba imesema kuwa, serikali ya Myanmar umetenda jinai za kivita dhidi ya Waislamu wa Rohingya na hivyo viongozi wake wanapaswa kuwajibishwa.
Baada ya hukumu hiyo, Daniel Feierstein Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya Uchunguzi wa Mauaji ya Kizazi sambamba na kuthibitisha kwamba kumetokea mauaji ya kizazi dhidi ya Waislamu wa Rohingya yaliyofanywa na serikali ya Myanmar amesema kuwa, mahakama hiyo imetoa uamuzi kwamba serikali ya nchi hiyo imefanya mauaji ya kimbari kwa makusudi dhidi ya Waislamu.
Karibu Waislamu laki nane wa jamii ya Rohingya wamekimbilia Bangladesh kutokana na mashambulizi makali yanayofanywa na askari wa serikali kwa wakishirikiana na Mabudha magaidi wa nchi hiyo na hadi sasa ripoti zinaonyesha kwamba, mauaji hayo bado yanaendelea.
Kwa mujibu wa ripoti zilizotolewa hivi karibuni, zaidi ya Waislamu elfu sita wameuawa kuanzia tarehe 25 Agosti mwaka huu na wengine wanaokaribia elfu tisa kujeruhiwa katika mashambulizi hayo ya kinyama.
No comments:
Post a Comment