Saturday, September 23, 2017

23 September 2017, Raia 6, 000 wa Kongo wamekimbilia Zambia kutokana na kuhofia usalama wao nchini humo

Vikosi vya serikali ya DRC vimekuwa vikiwaua raia, hali iliyosababisha wananchi wengi kukimbilia kaskazini mwa Zambia.

Zambia inahofia kuzuka migogoro kwani ni zaidi ya wakimbizi 6,000 wameikimbia DRC ndani ya mwezi mmoja.

Kwa mujibu wa habari,wakimbizi waliofika Zambia wamehojiwa na kusema kuwa wanaikimbia DRC kutokana na mauaji yanayofanywa na vikosi vya serikali nchini humo.

Mwakilishi mkuu wa UNHCR Zambia amesema kuwa serikali ya nchi hiyo imekuwa ikiwatesa wananchi kwa kuwaua,kuwachomea manyumba yao,ubakaji na vilevile kuvamia maghala ya chakula.

Viongozi wa Afrika Kusini wana nia ya kumteua kiongozi mstaafu atakayeweza kusaidia kutatua migogoro nchini Congo.

No comments: