Jaji Mkuu nchini Kenya ,David Maraga ameapa kuilinda na kuitetea sheria ya nchi hiyo hasa baada ya vitisho kutoka kwa wanasiasa.
Bwana Maranga ameyasema hayo katika mkutano mjini Nairobi na kuongezea kuwa yeye na majaji wengine hawatalazimika kumuunga mkono Rais Uhuru Kenyatta wala upinzani wake.
Kwa mujibu wa habari,bwana Maranga ametoa tamko hilo baada ya ombi la kumuondoa jaji mkuu kupelekwa katika mahakama ya juu ya Kenya.
Jaji Mkuu huyo pia amesema kuwa upande wao upo tayari kukabiliana na chochote kuhakikisha wanailinda katiba ya nchi hiyo.
Nje ya mahakama kuu,wafuasi wa rais Kenyatta walikuwa wakiandamana wakitaka majaji wakuu wawili wa juu waondolewe katika wadhifa wao.
Polisi walilazimika kupiga mabomu ya machozi.
No comments:
Post a Comment