Friday, September 22, 2017

22 September 2017,Agizo la Rais Magufuli la kujenga uzio kuzunguka machimbo ya madini ya tanzanite umeanza kutekelezwa

Siku moja baada ya agizo la Rais Dkt. JOHN MAGUFULI kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania - JWTZ kujenga uzio kuzunguka machimbo ya madini ya tanzanite eneo la Mererani, kikosi cha wataalamu wa Jeshi hilo kimeanza kukagua mipaka ya eneo hilo ili kuanza ujenzi.

Akizungumza mara baada ya kutembelea eneo hilo Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Michael Isamuyo amewaomba wananchi katika maeneo yatakayopitiwa na ujenzi huo pamoja na wamiliki wa migodi kutoa ushirikiano.

Ukaguzi huo umefanyika angani na ardhini kuzunguka machimbo ya tanzanite yaliyopo Mererani mkoani Manyara.

Mara bada ya kutembelea eneo hilo, Meja Jenerali ISAMUYO amesema wataanza kazi hiyo mara moja kama walivyoagizwa na Amri Jeshi Mkuu Rais John Magufuli.

Zoezi hili limeungwa mkono na wachimbaji wa madini katika eneo hili wakielezea kuleta manufaa kwao na taifa.

No comments: