Idara ya uhamiaji nchini imewakamata wahamiaji wasio na vibali nane raia wa Ethiopia waliokuwa wakisafiri kwenye lori kwenda mkoani Mtwara.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Kamishna wa Utawala na Fedha wa Idara ya uhamiaji Edward Chogero amesema wahamiaji hao wamekamatwa jana usiku katika eneo la Kongowe.
Kamishna Chogero amesema wahamiaji hao wamekamatwa kutokana na taarifa zilizopatikana kutoka kwa raia wema.
Amesema maafisa uhamiaji pia wamewakamata watanzania wanne na gari dogo aina ya Toyotà Passo ambayo inadaiwa kutumiwa na watuhumiwa hao wanaohusishwa na mtandao wa usafirishaji wa wahamiaji wasio na vibali.
Kamishna Chogero amesema mali za watu watakaobainika kujihusisha na mtandao huo zitataifishwa.
Wahamiaji wasio na vibali wapatao 5,700 wamekatwa tangu mwezi Januari hadi Juni mwaka huu.
No comments:
Post a Comment