Monday, September 18, 2017

18 September 2017,Viongozi wa Chama tawala Nchini Burundi wametupilia mbali ripoti ya UN

Chama tawala nchini Burundi kimelalamikia ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyoitaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) ifanye uchunguzi kuhusu jinai zilizofanywa na viongozi wa Burundi dhidi ya raia wa nchi hiyo.

Chama tawala Burundi kilieleza kuwa ripoti ya Umoja wa Mataifa inayosema kuwa viongozi wa Burundi wamehusika katika kukiuka haki za raia wake kuwa ni ripoti ya kisiasa na yenye lengo la kutoa pigo kwa chama hicho tawala. 

Kuhusiana na suala hilo Evariste Ndayishimiye Katibu Mkuu wa chama tawala cha Burundi amezishambulia kwa maneno Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya  kufuatia ripoti hiyo yenye kukinzana dhidi ya viongozi wa Burundi na kuitaja Ulaya na nchi za magharibi kuwa ni mashetani wa Ulaya.

No comments: