Sunday, August 6, 2017

6 August 2017, Makaburi ya halaiki yagundulika nchini Mali

Ujumbe wa usalama wa Umoja wa Mataifa (MINUSMA )nchini Mali imefanya ugunduzi wa makaburi ya halaiki katika kanda ya kaskazini ya nchi hiyo .

MINUSMA ulifanya shughuli ya ufukuaji wa makaburi hayo katika juhudi za kufanya utafiti kufuatia ripoti za kuwa na ukiukaji wa haki za kibinadamu katika kitongoji cha Anefis .

Kumekuwa na mapigano baina ya makundi kutoka jamii ya Tuareg katika wiki za hivi karibuni jambo aambalo limepelekea kuharibiwa kwa mkataba wa amani uliotiwa saini mwaka 205 .

Ujumbe huo hadi kufikia sasa umethibitisha ripoti 34 za ukiukaji wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na utumiaji wa watoto katika vita

No comments: