Thursday, August 31, 2017

31 August 2017, Watu 6 wafariki katika machimbo haramu ya madini Kusini-Mashariki mwa DR Congo

Watu 6 wamefariki katika maporomoko ya ardhi yaliotokea katika machimbo haramu ya madini Kolwezi Kusini-Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrais ya Congo

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyanzo vya habari  Kolezwi ni kwamba watu 6 wamefariki katika maporomoko ya ardhi ya machimbo ya madini Kolwezi, mgodi wa madini unaopatikana Kusini-Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Ajali hiyo imeripotiwa kutokea Jumanne wakati ambapo wachimbaji hao haramu walikuwa wakiendesha shughuli yao nya uchimbaji madini bila ya vibali.

Taarifa hiyo iliotolewa na gavana wa jimbo la Lualaba.

No comments: