Mwadui FC imeachana na Bushiri mwishoni mwa msimu uliopita taarifa hiyo imekuwa habari njema kwa Mwembeladu inayosaka huduma ya kocha huyo kwa muda mrefu.
Ofisa Habari wa Mwembeladu, Said Mussa alisema uongozi wa timu hiyo tayari umeshafanya mazungumzo ya awali na kocha huyo.
Mussa alisema lengo la kumsaka kocha huyo ni kuona timu yao msimu huu inafanya vizuri kwa kupanda daraja.
“Dhamira yetu ni kuona tunafanya vema katika ligi yetu msimu huu, ndio maana tunakosa usingizi kwa kumsaka Kocha Bushiri kila kona ili wachezaji wetu wapate mafunzo mazuri kutoka kwake,” alisema Mussa.
Kocha Bushiri alisema ni kweli amefanya mazungumzo na uongozi wa timu hiyo na anajipanga kufanya kazi na uongozi wa timu hiyo kwa mujibu wa makubaliano yao.
Alisema ataenda kuisaidia timu hiyo kwa vile mipango yake ni kufundisha soka Tanzania bara, lakini kutokana na mipango yake yakwenda huko haijakaa vizuri ameamua kutumia muda wake aliopo hapa kuwasaidia vijana wa timu ya Mwembeladu waliokuwa na hamu ya kufundishwa na yeye.
Admit Mwanasport
No comments:
Post a Comment