Afisa mmoja nchini Somalia ameshutumu jeshi la nchi hiyo pamoja na wafuasi wao kutoka nchi nyingine kuwaua raia tisa akiwemo mwanamke na mtoto mdogo.
Ali Nur Mohamed,Gavana msaidizi wa mkoa wa Shabelle ameviambia vyombo vya habari kuwa mauji hayo ya raia wasiokuwa na hatia yalitokea pale jeshi la Somalia pamoja na wanajeshi wengine kutoka nje,walipovamia shamba karibu na kijiji cha Bariire.
Kwa mujibu wa habari,wanajeshi hao walivamia shamba hilo siku ya Ijumaa na kuua watu tisa.
Hata hivyo makamanda wa jeshi nchini Soamlai hawakuwa na habari yoyote kuhusu operesheni ya namna hiyo.
Baadhi ya vyombo vya habari vinadai kuwa waliopoteza maisha ni watu kumi.
Afisa huyo amesema mauaji hayo yalikuwa ni ya makusudi na kuishutumu Marekani)
No comments:
Post a Comment