Msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara unaanza hii leo ambapo kwenye siku yake ya kwanza viwanja saba vitawaka moto na kesho kutakuwa na mchezo mmoja utakaochezwa hapa jiji DSM.
Kaimu katibu mkuu wa shirikisho la soka hapa nchini (TFF) Wilfred Kidau amesema wanataka ligi hiyo iendeshwe kwa haki na usawa na hakuna kuipendelea timu yeyote.
Timu kumi na sita zinashiriki ligi hiyo huku kukiwa na timu mpya tatu zilizopanda daraja msimu huu ambazo ni Singida United, Njombe Mjii na Lipuli FC ya Iringa.
Enock Bwigane
No comments:
Post a Comment