Friday, August 25, 2017

25 August 2017, Kwa mara ya kwanza mfungwa mwenye ngozi nyeupe kunyongwa Florida

Florida kwa mara ya kwanza katika historia imetoa adhabu ya kifo kwa mfungwa mzungu kwa kosa la kumuua mwanamume mweusi.

Mfungwa huyo aliuawa Alhamisi iliyopita katika moja ya gereza la serikali.

Mark James Asay mwenye umri wa miaka 53 amehukumiwa kifo na kuuawa baada ya kumuua Rober Lee Booker mwenye umri wa miaka 34 na Robert McDowell mwenye umri wa miaka 26 mnamo mwaka 1987.Bwana James alipangiwa kuuawa kwa kutumia sindano.

Kwa mujibu wa habari,toka adhabu ya kifo irejeshwe mwaka 1976 Florida ni takriban watu weusi 18 wameuawa kwa makosa ya kuwaua watu weupe.

Adhabu ya kifo kwa kutumia sindano aliyopewa Asay na ni mara ya kwanza kutumika katika historia ya Marekani ni adhabu ya kwanza kutolewa Florida ndani ya miezi 18 iliyopita.

Hata hivyo wale wanaopinga adhabu ya kifo wamekuwa wakipingwa watengeneza sindano hiyo kutoisambaza serikalini.

Ripoti zinaonyesha kuwa bwana Asay na rafiki zake walikuwa wamelewa usiku wakati alipompiga risasi Booker aliyekuwa akitembea mtaani.

No comments: