Waziri mkuu wa zamani nchini Libya Ali Zeidan ameripotiwa kuvamiwa na kutekwa nyara katika hoteli alimokuwa na watu waliojihami kwa silaha usiku wa Jumapili jijini Tripoli .
Zeidan alikamatwa na kuepelekwa katika eneo lisilojulikana .
Hadi kufikia sasa hamna kundi lililotangaza kuhusika na utekeji nyara huo .
Taarifa pia zafahamisha kwamba sio mara ya kwanza kwa waziri huyo wa zamani kutekwa nyara .
Alipokuwa waziri mkuu mwaaka 2013 ,Ali Zeidan aliwahi kutekwa nyara wafuasi wa chama cha mapinduzi cha Libya na kuachiliwa huru baada ya masaa kadhaa ya kushikiliwa mateka
No comments:
Post a Comment