Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa onyo kwa mtumishi yeyote wa umma ama mtu atakayekutwa na dawa za serikali kwenye duka lake la dawa.
Akiwahutubia wananchi Wilayani Sikonge Waziri Mkuu Majaliwa amesema kuwa serikali imedhamiria kuondoa kero za huduma za afya kwa wananchi kwa kuchukua hatua kali kwa yeyote atakayetumia fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya kuboresha huduma za jamii.
Aidha Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa amewataka watalaamu wa mifugo wilayani humo na mkoa wa ujumla kutoa elimu ya ufugaji bora kwa wafugaji na kutenga maeneo ya malisho yenye miundo mbinu.
No comments:
Post a Comment