Saturday, July 29, 2017

29 july 2017, KAGOMA KUOGA KWA MUUDA WA MIAKA 43

Kailash Sing ambaye hivisasa ana umriwa miaka 71 hajawahikuoga wala kukata ndevu zake tangu alipooga kwa mara mwisho kabla ya sherehe ya harusiya kumuoa mkewe,mwaka 1974.

Sing anaelezea sababu ya msimamo wake huo kuwa nishartila utabirialiopewa na mmoja wa kiongoziwa diniya Hindu kuwa atakapopata mtoto wa kiume,basimtoto huyo atakuwa mwenye mafanikio makubwa sana kwenye maisha yake na atakuwa tajirisana.

Nimiaka 43 imepita lakini Sing anaendelea na msimamo wake wa kutooga mpaka pale atakapofanikiwa kupata mtoto wa kiume.

Sing ana jumla ya watoto saba wa kike lakini juhudi zake zote za kupata mtoto wa kiume bado hazijazaa matunda.

Mkewe ambaye sasa ana umri wa miaka 66, alishawahi kujaribu kuweka mgomo wa kutoa unyumba mpaka Sing atakapooga lakinimgomo huo uligonga mwamba kwani Sing hakujali chochote na matokeo yake mgomo huo uliisha.

Majirani na watoto wamekuwa wakimtania na kumtupia maneno ya kejeli mzee Sing ambaye amekuwa akipuuza kila anachoambiwa mpaka pale ndoto yake ya kuwa na mtoto wa kiume itakapotimia.

Familia yake nayo imewahi kujaribu kutumia maguvu kumuogesha kinguvu Sing kwenye mto lakini Sing alifanikiwa kuwazidi nguvu na kukimbia akisema kuwa niheri afariki kuliko kuvunja sharti litakalomwezesha kupata mtoto wa kiume.

Kinachomfanya Sing awe anatoa harufu kali ni kazi yake ya ufugaji ambayo huifanya akizunguka kuwalisha majani ng'ombe wake kwenye kijiji chake cha Chatav ambapo hali ya hewa yake niya joto kali wakatimwingine kufikia joto la nyuzi47C.

Mbaliya kutooga,Sing hajazikata ndevu zake na wala kuzinyoa nywele zake ambazo hivisasa zimefikia urefu wa mita 2

Ilikuusafisha mwiliwake,Sing huota moto kila siku jioni huku akisali kumuomba mungu wake wa Kihindu,Shiva.

'Wakati ninapoendesha baiskeli kwenda kwenye shughulizangu,watoto wamekuwa wakitania na kunipiga kelele kuwa siogi,hawaelewi kwanini nafanya hivi sitabadili uamuziwangu mpaka nitakapopata mtoto wa kiume",alisema Sing.

Huenda mwanaume huyu wa nchini India akawa ndiye mtu mwenye kunuka kuliko watu wote duniani kwani hajaoga wala kukata ndevu zake kwa miaka 43 sasa,sababu ya kufanya hivyo niiliaweze kupata mtoto wa kiume.

No comments: