Thursday, July 27, 2017

27 july 2017, Kibadeni atua Mbao FC

Zikiwa zimebakia takribani siku 10 kufungwa kwa dirisha la usajili wa msimu mpya wa ligi kuu Tanzania Bara, timu ya Mbao FC imeendelea kujiimarisha kwa kumsajili mchezaji chipukizi Suleiman Kibadeni kutoka Zanzibar kuwatumikia wakata mbao hao kwa
miaka miwili kuanzia hivi sasa.

Timu hiyo ilinusurika chupu chupu kushuka daraja katika msimu uliyopita ambapo hivi karibuni iliondokewa na nyota wake watano baada ya kuonekana wazuri katika vilabu vingine vya hapa nchini Tanzania.

Wachezaji hao ni makipa Benedict Haule na Emmanuel Mseja, kiungo Salmin Hoza waliokwenda Azam FC, beki Jamal Mwambeleko waliokwenda Simba na kiungo Pius Buswita aliyekwenda Yanga.

Chanzo Eatv

No comments: