Wednesday, July 26, 2017

26 july 2017, Watu 43 wafungwa kifungo cha maisha nchini Misri

Mahakama moja nchini Misri imetoa adhabu ya kifungo cha maisha kwa watuhumiwa 43 waliohusika na ghasia za 2011 baada ya kuondolewa kwa Hosni Mubarak kufuatia shughuli zake za uasi .

Wakati huo huo mahakama hiyo iliwatoza washutumiwa hao faini ya takriban dola milioni moja .
Vile vile mahakama hiyo imewapa vijana wengine 9 adhabu ya miaka 10 gerezani .

Hata hivyo watuhumiwa hao wana fursa ya kukata rufaa .

Mnamo mwaka 2011 ghasia zilizuka baina ya waandamanaji na vikosi vya usalama na kupelekea vifo vya watu 18 na kadhaa kujeruhiwa

No comments: