Thursday, January 25, 2018

25 January 2018,Aguero huenda akajiunga na Atletico Madrid

Manchester City huenda ikaingia katika makubaliano na Atletico Madrid kubadilishana mshambuliaji raia wa Argentina Sergio Aguero, mwenye umri wa 29, ili kwa upande wake imchukue Antoine Griezmann, raia wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 26 katika msimu ujao wa joto. (Sun)

Lokomotiv Moscow imeifuata Liverpool kumtaka kumsajili winga mwenye umri wa miaka 23 Lazar Markovic. Msimu uliopita Mserbia huyo alichukuliwa kwa mkopo huko Sporting Lisbon na Hull City. (Mirror)

Chelsea imekubaliwa ombi lenye thamani ya pauni milioni 44, na marupurupu kwa msahmbuliajo wa Roma Edin Dzeko, na full beki raia wa Brazil Emerson Palmieri. (Guardian)

Kipa raia wa Uhispani wa Getafe Vicente Guaita, mwenye umri wa miaka 31, amefuzu ukaguzi wa kiafya huko Crystal Palace - lakini mazungumzo yangali yanaendelea kuhusu iwapo atajiunga na timu hiyo sasa au katika msimu wa joto. (Mail)

Brighton imewasilisha ombi la pauni milioni 6 kwa mlinzi wa Bristol City Aden Flint, aliyedhihirisha umahiri wake katika mashndano ya taji la Carabao. (Argus)

Klabu ya Ufaransa Monaco imekubali kumuuza mshambuliaji raia wa Argentina Guido Carrillo, kwa Southampton kwa pauni milioni 19.2. (Telegraph)

Sevilla imekubali makubaliano ya kumsajili mchezaji kiungo cha kati wa Swansea City Roque Mesa, mwenye umri wa miaka 28, kwa mkopo kwa muda uliosalia. (Marca - in Spanish)

No comments: