Wednesday, December 27, 2017

27 December 2017,Wazayuni waendelea kuwashambulia waandishi wa habari nchini Israel

Wanajeshi makatili wa Kizayuni ambao wanaikalia kwa mabavu Quds Tukufu yenye Kibla cha Kwanza cha Waislamu wamewashambulia na kuwajeruhiwa waandishi wa habari zaidi ya mia moja tangu lilipozuka wimbi la kulalamikia uamuzi wa rais wa Marekani wa kuitangaza Baytul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala pandikizi wa Israel.

Shirika la habari la Mehr limetangaza habari hiyo leo na kuyanukuu mashirika ya haki za binadamu yakisema kwamba, Wazayuni wamekuwa wakiwashambulia kwa makusudi waandishi wa habari tangu lilipozuka wimbi la kupinga kitendo cha rais wa Marekani Donald Trump cha kuitangaza Quds kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni na kwamba kati ya waandishi hao walioshambuliwa na Wazayuni, 20 ni wanawake.

Wanajeshi makatili wa Israel wanatumia kisingizio cha kukabiliana na maandamano ya Wapalestina kuwashambulia kwa makusudi waandishi wa habari kwa risasi hai na za plastiki pamoja na mabomu ya kutoa machozi, kuwamwagaia pilipili na kuwapiga kwa marungu.

53 kati ya waandishi hao wamejeruhiwa wakati walipokuwa wanaripoti maandamano ya Wapalestina ya kumlaani Donald Trump huko Baytul Muqaddas pekee.

Hii ni katika hali ambayo idadi kubwa ya waandishi wa habari wamekamatwa na wanajeshi wa Israel wakati waandishi hao wakiwa katika kuripoti matukio mbalimbali huko Palestina katika kipindi hicho.

Kamati ya kulinda usalama wa waandishi wa habari ya Palestina imesema kuwa, lengo la utawala wa Kizayuni ni kuzuia waandishi hao wasiwafichulie walimwengu jinai kubwa zinazofanywa na Israel dhidi ya wananchi wa Palestina.

No comments: