Thursday, November 30, 2017

30 November 2017,Zaidi ya viongozi 80 kutoka Afrika na Ulaya waketi kuzungumzia uchumi na Uhamiaji nchini Ivory Coast

Zaidi ya viongozi 80 kutoka Afrika na Ulaya wamekutana nchini Ivory Coast siku ya Jumatano ya jana

Kwa mujibu wa habari,viongozi hao wamekutana katika mji mkuu wa Abidjan kwa muda wa siku mbili kuzungumzia masuala ya uchumi pamoja na uhamiaji.

Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Macky Sall wa Senegal,Emmanuel Macron wa Ufaransa,Muhamadu Buhari wa Nigeria.

Kabla ya rais Macron kuhudhuria mkutano huo alipitia Burkina Faso kuzungumzia suala la kupambana na ugaidi.

Macron anaonekana kutengeneza uhusiano mzuri na viongozi mbalimbali barani Afrika.

No comments: