Thursday, November 30, 2017

30 November 2017,Serikali yanasa zaidi ya kilo Sita za madini ya dhahabu

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya DSM kitengo cha makosa ya rushwa na uhujumu uchumi kimetaifisha kilo zaidi ya sita za madini ya dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 507 iliyokuwa imepangwa kusafirisha kwa njia za magendo kutoka Dar es salaam kwenda Zanzibar.

Hatua hiyo inafuatia hatua ya serikali kushinda kesi dhidi ya wafanyabiashara wawili wa jijini waliokuwa wakishirikiana na mchimba madini kutoka Geita Kalangalala Mashaka Lucas.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu,Huruma Said watuhumiwa wamekiri kosa chini ya sheria ya makosa ya uhujumu uchumi namba 67 ya mwaka 2017.

Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Biswalo Mganga amethibitisha kutaifishwa kwa miche mitano ya dhahabu na kuwataja wafanyabiashara wakazi wa Dar es salaam waliokuwa wakishirikiana na mfanyabiashara kutoka Geita kuwa ni Jaffar Hussein na Latiff Mohamed.

No comments: