Monday, November 27, 2017

27 November 2017,Makosa ya usalama barabarani kwa siku 12 yaingiza zaidi ya bilioni mmoja serikalini Jijini Dar es salaam

Makosa ya  usalama barabarani  yaingiza  serikalini Sh bilioni 1.11 kama tozo za makosa mbalimbali ya usalama barabarani kanda maalum ya Dar es salaam  kwa siku 12.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini hapa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Lazaro Mambosasa alisema fedha hizo zimekusanywa kupitia kikosi hicho ikiwa inaendelea na uperesheni ya ukamataji wa makosa ya usalama barabarani.

Alisema jumla ya makosa yaliyokamtwa ni 36,353 huku magari yaliyokamatwa yakiwa 33,444, pikipiki zilizokamatwa ni 795, daladala 12,197, magari mengine binafsi na malori 21,247.

Mambosasa alisema jumla ya waendesha pikipiki 92 walifikishwa mahakamani kwa makosa ya kutovaa kofia ngumu na kupakia abiria zaidi ya mmoja. Aidha Mambosasa amewatangazia wananchi kutumia namba 41.59.7.174/tms kwa simu zao za mikononi zenye uwezo wa intaneti kwa kutumia kitufe cha kuingia kwenye mtandao google Browser kwa maulizo ya faini zilizoandikwa kwa mashine za kielektroniki Traffic Management Systems (TMS).

Vile vile amewaasa madereva kulipa faini ndani ya muda wa siku saba ili kuepukana na usumbufu wa kukamatwa pamoja na ongezeko la tozo za faini.

Katika tukio jingine jeshi hilo linawashikilia watuhumiwa 140 kwa makosa mbalimbali ya uhalifu pamoja na dawa za kulenya.

Alisema Polisi wamekamata magunia manne ya bangi, kete 147, puli 73, misokoto 55, pamoja na pombe haramu ya gongo ipatayo lita 300 na mitambo sita ya kutengenezea gongo.

No comments: