Sunday, November 26, 2017

26 November 2017,Wahamiaji haramu 31 wafa maji katika pwani ya Libya baada ya mashua yao kuzama

Wahamiaji haramu 31 wafa maji na wengine 35 waokolewa baada ya mashua yao kuzama katika  pwani ya Libya

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na polisi ya pwani ya Libya ni kwamba wahamiaji haramu 31 wamefariki na wengine 35  wamokolewa baada ya mashua yao kuzama nchini Libya.

Msemaji wa polisi ya kulinda pwani Libya kanali Ayub Qassem amefahamisha Jumamosi kuwa operesheni ya kuwaokowa wahamiaji hao ilifanyika katika eneo la Castelverde Mashariki mwa Tripoli.

Kanali huyo amefahamisha kuwa miongoni mwa watu waliookolewa walikuwemo watoto.

No comments: