Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Louise Mushikiwabo asema kuwa serikali inapanga kuwachukuwa wahamiaji 10 000 wanaoomba hifadhi nchini Israel.
Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Louis Mushikiwabo amesema kuwa Rwanda itawachukuwa wahamiaji wapatao 10 000 kutoka katika mataifa tofauti wanaoomba hifadhi nchini Israel.
Wizara ya mambo ya nje ya Rwanda imethibitisha kuwa serikali ya Rwanda na ile ya Israel zipo katika mazungumzo ili kukubaliana masharti kuhusu wahamiaji hao watakaopoklewa nchini Rwanda.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amefahamisha Jumapili kuwa itawafukuza wahamiaji wapatao 40 000 na kufunga kituo kilichokuwa kikiwazuia wahamiaji Kusini mwa Negev.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na jarida la Haaretz la Israel, serikali ya Israel itatoa kiwango cha dola 5000 kwa Rwanda kwa kila muhamiaji mmoja iwapo Rwanda itakubali kuwapokea.
Wengi miongoni mwa wahamiaji walioko nchini Israel ni raia kutoka Sudan na Eritrea.
No comments:
Post a Comment