Wednesday, November 22, 2017

22 November 2017,Korea Kaskazini yapiga marufuku mziki na pombe nchini humo

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amepiga marufuku mashirika ya burudani yakiwemo yale ya pombe na muziki.

Kwa mujibu wa habari,Korea Kaskazini imefanya hivyo kwa nia ya kudhibiti uchumi wa nchi hiyo hasa baada ya vikwazo vilivyowekwa na Umoja wa mataifa,
Korea Kaskazini imewekewa vikwazo vingi kutokana na kukiuka masharti na kuendelea kutengeneza makombora ya nyuklia.

Wananchi nchini humo wamekuwa wakijaribu kuishi ndani ya matakwa ya serikali.

Mbali na kuwa vigumu kwa wananchi wa Korea Kaskazini kusafiri nje ya nchi,utumiaji wa mitandao ya kijamii bila idhini ya serikali nao umedhibitiwa vilivyo.

Hata hivyo Pyongyang haionyeshi dalili zozote za kaucha kufanya majaribio ya makombora ya nyuklia.

No comments: