Saturday, November 11, 2017

11 November 2017, Watu kumi wanaodaiwa kuwa magaidi wauawa nchini Misri

Watu  kumi   wanaodaiwa kuwa  magaidi wameripotiwa kuuawa baada ya mashambulizi ya anga kufanyika nchini Misri.
Kwa mujibu wa habari,helikopta za kijeshi zimeshambulia ngome zote za magaidi katika mji wa Sheikh Zuweid Misri.
Maafisa wa polisi  pia wamefanikiwa kutengua mabomu yaliyokuwa yametegwa katika sehemu mbalimbali mjini humo.
Toka mwaka 2013 baada ya rais wa nchi hiyo kuondolewa madarakani kwa kupinduliwa,Misri imekuwa na matatizo katika usalama wa wananchi.
Hata hivyo jitihada zinaonyeshwa kwa kina katika kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani kama ilivyokuwa zamani.

No comments: